Friday, August 31, 2012

Wanaume wanaume wanaume mnakera!

Hata salamu leo sitaki,

Hivi we mwnaume wa aina gani?? Umekaa na mkeo au mpenzi wako anapita mwanamke mwingine unageuka na kumtolea mimacho tena unaduwaa kabisa, hivi we hauna haya na kama huyo mwanamke atakuwa amekaa meza ya nyuma basi ndo kabisaaaaa kila saa unageukageuka. Hakyanani mi nikikuona nitakumwagia maji.

Haya kwa wale waendesha magari, utakuta mpenzi wake yuko pembeni  na yeye anaendesha sasa akimuona msichana tu pembeni anapita au kasimama barabarani basi kosa lazima aangalie mara mbilimbili, vipi baba? utapata ajali bureee,

Najua wengi hapo mnanijibu "aaah si fahari ya macho?" Sawa we unaona fahari ya macho lakini hiyo inamuumiza mwenzako.Na yeye akipita mwanaume mwenye mvuto aangalie?? Au akipita mwanaume ana gari ya nguvu kuliko hiyo Vits yako aangalie??Najua na nyie inawauma sana, sasa kwa nini umfanyie mwenzio? Mjini sasa hivi kila mtu mzuri kila mtu anajua kuvaa utaangalia wangapi? Jifunze kuridhika na kujivunia ulichonacho, kama unamuona hajapendeza mpendezeshe ati! wannakwambia USIONE VYAELEA UJUE VIMEUNDWA hao unaowaona warembo wamerembeshwa sasa hata ukisema umchukue huyo mrembo usipomgharamia atakongoroka vilevile.

Na niwaambie ukweli wengi wanalalamika ooh mi demu wangu hayupo serious kwenye mahusiano yetu sijui nini...sasa ye ashakuona mwanaume macho waluwalu unadhani atakaa anaona bora na yeye aendelee na mambo yake manake asije akalia bure mwisho wa siku.

Hata kama atapita mrembo gani angalia tu kama ambavyo jicho halina pazia endelea na mambo yako, kuduwaa na kugeuzageuza shingo huo ni ushamba!! Unamwaibisha mpenzio.

Najua hili limewauma sanaaa sasa nasema hivi nendeni kwa hospitali wote mkachome ganzi
Mi ndo nisharopoka

Tuesday, August 28, 2012

Unatembea na Mume wa Mtu? Soma hapa

Sasa leo nawaibukia wanawake wanaotembea na waume za watu,

Utakuta mtu anaanza mahusiano na mwanaume ilihali akijua kabisa ni mume wa mtu. Mwanaume wa watu kamweleza ukweli kabisa kuwa mimi nimeoa ila nataka kuwa na wewe we mwanamke na nyege zako na tamaa zako au pengine na wewe umempenda unakubali ila ninapokwazika mimi ni pale mwanaume akikwambia muda umeenda wacha niwahi home we unanuna sasa unanuna ili iweje? Ulitaka alale kwako? Si alishakwambia ana mke na unajua lazima alale kwa mkewe, kama unataka mtu wa hivyo basi tafuta wa kwako ila kama umeamua kuwa na mume wa mtu basi heshimu familia yake, usitake kumkwaza wala kumvurugia ndoa. Kwanza we huoni raha kama mwanaume atakuwa na furaha muda wote kuliko wasiwasi? Manake ukimvurugia ndoa hata wewe utamkosa asikudanganye mtu hakuna mwanaume asiyempenda mkewe, watakwaruzana mwisho wa siku watasuluhisha wataendelea na maisha shosti we utabaki kuumbuka.

Maji ukiyavulia nguo sharti uyaoge na ukipenda boga penda na ua lake umependa mume wa mtu basi heshimu familia yake!

Jifunze kula na kipofu shoga hahahaaaaa lako hilo!

Hii imemtokea rafiki yangu wa karibu sana, ila nashukuru ndoa yake haijavunjika.

Linauma, choma ganziiiiiiiiiiiiiiiiii

Monday, August 27, 2012

Jifunze kunyonya bwana we vipi?

Habari zenu wapendwa,

Leo nakuja kwa wale wasiojua kutumia midomo yao vizuri pale wanapowanyonya wapenzi wao,
Kwanza unaponyonyana mate jitahidi kuzuia meno yako kwa sababu meno yakingonganya na ulimi wake au fizi zake lazima aumie hata ile radha yote inaisha

Pili, hapa zaidi ni kwa wanawake unaponyonya mashine ya mzee wako tafadhali narudia tena tafadhali tumia ulimi wako kuziba meno ya chini na meno ya juu maranyingi yanafichwa na lips za upande wa juu. Mwanaume anaumia sana pale ukiwa unamnyonya halafu meno yako yamguse kwenye uume wake au yamsugue sema wengi hawasemi na ndio maana mwingine anaweza tu kukukatalia usimnyonye. Sasa hujiulizi kwanini akate kunyonywa? Kuna mtu ambaye hapendi raha? Asikwambie mtu huyo anaona unamuumiza ndo maana hataki umnyonye.

Kingine, haswa kwa wanaume maziwa ya mwanamke ni kiungo kizuri sana cha kuleta msisimko ila sasa kuna mijitu mingine inanyonya utadhani mbuzi yani atanyonya kama anataka kukata nyonyo aaaah we vipi bwana unamuumiza mwenzio kwani ugomvi? tumia ulimi wako kulamba chuchu na hata kama unanyonya hutakiwi kuvuta. Unanyonya huku ulimi wako unauchezea kwa chuchu.

Pia unapomnyonya mwanamke sehemu zake nyeti tafadhali tena tafadhali sana usitumie nguvu wala usinyonye kwa kuvuta unamuumiza na hasikii raha yoyote ndo maana mwingine anakuwa hataki au ukishaanza tu kumnyonya haraka anakutoa, we unadhani kwanini ? ni kwasababu unamuumiza hakuna mtu asiyependa kunyonywa kunyonywa kuna raha yake bwana.


Pamoja na yote meno unaweza kuyatumia kuleta msisimko kwa kufanya kama unataka kung'ata lips za mpenzio au hata sehemu nyinginezo, ila sio unang'ata sasa manake kuna mijitu mingine itataka ikung'ate kabisa.
Tumia ulimi wako vizuri bwana alah!

Mi ndo nisharopoka hivyo, Kama linauma kama kawa choma ganzi tu!

Thursday, August 23, 2012

Acha kumjaribu mpenzio! Acha pozi


Kwanini unamjaribu mpenzio? Ili iweje? AU ndo unataka uone udhaifu wake? Na ukisha uona nini kinafuata?  Acha utoto huo ni ujinga, hata siku moja usimuwekee mitego mpenzi wako kwa lengo la kujua alivyo kama unataka kujua nyendo zake basi we mfuatilie tu na umchunguze ila usimuwekee mitego.
Mfano utakuta mtu anapanga na marafiki zake ili wamtongoze huyo mpenzi wake tena hii ipo Pande zote kwa wanawake na wanaume, eti  anataka ajue kama huyo mpenzi wake atamsaliti au la! Sasa ina maana we humuamini au?
Nakuambia ukweli ukijaribu kufanya hivi jua huo uhusiano wenu haufiki mbali sababu ndo utakuwa mchezo wako na mwisho wa siku mpenzio atakereka, tena mwingine akijua ndo kabisa anakuacha na huyo rafiki yako uliyemtuma anatembea naye. Kwanza usipende sana kuwaamini marafiki kwenye mapenzi  kiasi cha kumtuma akamtongoze mpenzio kwasababu anaweza fika huko akapewa mambo motomoto akanasa sasa hapo kuna mawili utaachwa na wao wataendeleza uhusiano au utaanza kudanganywa kumbe wao wanaendelea kumega tunda wewe huna habari.  Na asikwambie mtu huyo mpenzio akijua umemuwekea mtego huo hata akupende vipi atakuacha tu.
Pia kuna wale watu wengine ambao sielewi ni pozi au ni nini? Mfano utakuta mwanaume kwa siku kama mbili hivi hampigii mpenzi wake simu na akipigiwa hapokei au akipokea anamkaripia, na mwanamke wa watu wala hachoki wala hachukii anajua mpenzie kabanwa siku wakiongea sasa mwanaume anaanza kujitapa nilikuwa nimekuchunia makusudi ili nikuone presha inavyokupanda khah!! Huu ni utoto ndugu yangu na una impact mbaya sana kwenye mapenzi ukimkuta mtu ambaye uvumilivu wake mdogo lazima akuache, hebu acha mara moja hii tabia kama kweli unampenda mpenzio!

Mapenzi ni kuaminiana siyo kujaribiana na kutesana umeona hakufai basi muweke wazi ajue kuliko kupotezeana muda.
Ndio nimekulenga wewe nitupie tu mawe ila lazima uambiwe ukweli


UJUMBE: KAMA WEWE UNANIONA WA NINI WENZAKO WANAJIULIZA WATANIPATA LINI

Tuesday, August 21, 2012

Si Kila Kitu Unaomba

Si kila unachoomba unapewa kwa moyo mweupe vingine unapewa kwa moyo wenye giza, tena huwezi jua mtu anaumia kiasi gani kukupa hicho kitu sema kutokana na mazingira mliyoishi, mapenzi na heshima anaamua tu kukupa.

Kabla hujaomba kitu kwa mtu fikiria mara mbili, watu wengine wanamioyo ya kutoa hashindwi kukupa wewe chakula chake chote kisha yeye akashinda njaa. Angalia kitu gani unaomba kwanza na huyo mtu unayemuomba ni nani na uwezo wake wa kukupa. Anaweza kukupa ila moyoni anasononeka sana imemuuma sana moyoni sasa usitegemee utabarikiwa na hicho kitu alichokupa kama ni pesa basi hutaifanyia hata kitu cha maana, kama ni  gari basi hata wiki nyingi utaona ajali, kama nyumba utashangaa ajali za moto hazikuishi na ikiwa ni mpenzi sijui hapo inakuwaje.

Kuwa makini

Sijamlenga mtu hili ni wazo tu limenijia, msinirushie mawe

Saturday, August 18, 2012

Wanawake Tuache Gubu

Wanawake wengi walio kwenye ndoa au wanaoishi na wapenzi wao huwa wanakosea kitu kimoja, GUBU

Gubu ni nini? Ni ile tabia ya kuongea sana kwa shutuma. Utakuta mume akirudi tu anaulizwa, ulikuwa wapi? ulikuwa na nani? unafanya nini? mbona umechelwa? tena hapo mwanamke kanuna. Jamani jamani jamani mwanaume hata hajapumzika hajapata hata kikombe cha maji? maneno yanaanza??Kwa mtindo huu ndo maana wanaume wengi wanaona bora tu wachelewe kurudi wapite baa wanyweeeee ili akija home hata useme nini yeye hakusikii analala tu, na kwasababu hii wanaume wengi hawapendi kutoka na wake zao manake wakitoka maneno njia nzima mwanamke hayamuishi. Punguza shosti, gubu linakera.

Ni vizuri kujua mahali aliko au alipokuwa mumeo ila tumia njia za busara kumuuliza, akirudi mpokee vizuri muandalie maji ya kuoga, chakula akishapumzika ndo unaweza kumuuliza tena si kwa ugomvi.

NA sio tu kwa mumeo pia kwa mtu yoyote yule acha kuongeaongea sana ndo nyinyi ambao mnakimbiwa na ndugu, hata salamu kutoka kwao hupati wala hata siku moja huoni mtu akija kuwasalimia. Yote hii inasababishwa na gubu, Punguza bibie

Kama linauma choma ganzi, mi ndo nisharopoka!

Chezea JT wewe!!

Wednesday, August 15, 2012

USHAURI: Mawasiliano yamepungua



SWALI: Mambo jesca? yah nimetembelea blogspot yak an kiukwel imenivutia thus why nimeamua nikuandike hii coz it seems lyk ur a wise woman Nina mpenz wang mwak mmoj na nusu sas tatzo ni kwamb nowdays kachange tofaut na zaman nikimtxt ajib txt on tym or mda mwngne acjb kabsa imefika hatua nicpo mtafuta anawez kuuchna hat wik then nikimuuliz tatzo nin or mara kuwasilian san hain maan kam nakupend an non sens reason vp jessy kun mapenz kwel hap? Frankly speakin nampenda sana tena sana an anajua may b ndo maana ananisumbua nisaidie ki2 kimoja ths tym natka nimwache but nashndw nifanyej ili nweze kumsahau? Coz npo kidato cha mthan wa taifa an mda mwing ananipa strec zinazonpa headache

JIBU: Pole sana David ni wazi huyo msichana anakuchakachua kwa kawaida huwezi kumuignore mpenzi wako kihivyo so niwadhi anakusaliti, ila usichukue maamuzi ya kumuacha ghafla jaribu kuchunguza ni kitu gani haswa kinamfanya asiwe karibu na wewe pia jaribu kuchunguza kama kuna mtu anamega tunda lako au lah! pengine hana mpenzi mwingine ila kuna vitu unamkera kila ukiongea naye au unapokuwa nae ndo maana anakukwepa. Njia nzuri ni kukaa chini na kuzungumza, ila kama ni mwanafunzi kama ulivyosema maliza kwanza mitihani manake shule ndo mpango mzima, manake ukifeli halafu mwanamke pia ukamkosa utajikuta unadata, so tuliza akili yako we endelea kuwasaliana nae tu kama kawaida ukimaliza sasa mitihani mwite  ikiwezekana mtoe out mwende sehemu yenye utulivu na muongee mwambie unavyojisikia na umpe uhuru wa yeye aeleze anavyojisika na anavyokuchukulia wewe, mimi naamini hapo mtapata suluhisho kama mtaachana au mtarekebisha makosa yenu, ila usikurupuke kumwacha!

Hayo ndo maoni yangu. Kama kuna mwingine atakuwa na ushauri zaidi basi tiririka hapo chini kwenye comment 

Tuesday, August 14, 2012

Marioo wamezidi mjini!

Bado sijajua undani wa hili jina na origin yake ila ndilo jina linalotumiwa kumwita kijana mdogo anayekuwa na mahusiano na mwanamke mtu mzima ambaye anaweza hata kumzaa, mara nyingi 'marioo' huyu anafuata pesa tu kwa huyo mwanamke wala si kingine na pembeni atakuwa na msichana mwingine ambaye ndiye atakuwa anampenda

Sasa hivi mjini hawa watu wamejaa sana, tena sikuhizi hawaoni hata aibu wanajionesha waziwazi. Utakuta kijana mdogo sana lakini anampetipeti jimama huyo hadi utabaki mdomo wazi na hapo pengine anajua kabisa labda huyo mwanamke ni mke wa mtu lakini wala hashtuki, kwanini ashtuke wakati yeye yupo pale kuchuma pesa? Utakuta amekabidhiwa gari aendeshe sasa hizo fujo mtaani kwao hapakaliki mradi tu mbwembwe, sasa ndugu yangu kama wewe ni marioo jua upo hatarini sana kuhariibikiwa na maisha yako hizo pesa unazozifuata utakuja kuziona chungu, wenzako yamewatokea na tumewaona sasa itakuwa zamu yako.

Acha umarioo wewe fanya kazi, mwanaume atakula kwa jasho we vipi????

Usibweteke

Kuna watu huwa wananishangaza sana yani wao wenyewe wanategemea wapenzi wao wawafanyie kila kitu gharama za matumizi zote wanawaachia wapenzi wao wao hata kusema kujishughulisha na kitu hawana wapo tu! Mradi mpenzi wake anapesa basi yeye anachojua ni matumizi tu, Sio vizuri hata kama mumeo anapesa lazima ujitahidi nawewe ujishughulishe na kitu chochote japo lotion yako ununue kwa pesa yako mwenyewe au we huoni mateso kila ukitaka kitu unaanza kuomba' Dear lotion imeisha'

Vitu vidogo jifunze kununua mwenyewe, kama huyo mpenzi wako anahela sana na anataka maendeleo yako basi hata kama hujasoma atakufungulia biashara sababu atakuwa ashaisoma akili yako ashajua kuwa si mtu wa kubweteka lakini wewe ukijifanya wa kwenda salon na shopping za nguo kwa wingi unadhani atakufungulia biashara yoyote? Ataona kama anapoteza pesa zake bora awe anakupa hivyohivyo tu sasa haya si mateso?

Loh! shostito kama limekuuma choma ganzi! ila mi ndo nisharopoka

Uzuri na Ubaya wa Zawadi kwa mpenzi wako!

Zawadi inaweza kuwa kitu chochote cha gharama au si cha gharama, thamani yake ipo kwa yule mtu anayepewa.

Uzuri wake ni upi?
Kwenye mapenzi zawadi ni kiungo muhimu sana, sio lazima umletee mpenzi wako kitu cha gharama saaaana unaweza ukanunua hata ua au card yenye maneno mazuri ukampelekea au hata chocolate, hii itamfanya ajione kuwa anakumbuka basi kwa kiasi fulani upendo wake utaongezeka kwako ataona anapendwa sana hivyo naye atajitahidi kurudisha mapenzi kwa nguvu zake zote na hapo kwa asilimia fulani mapenzi yenu yatakua.

Ubaya wake ni upi?
Kuna baadhi ya watu hupenda sana kuwapa wapenzi wao zawadi mfano kila akisafiri lazima amletee pafyumu fulani japo sio mbaya, kwahiyo yule mwanamke anakuwa ashajijengea mpenzi wangu mimi akisafiri akirudi lazima ana pafyumu mkononi, sasa hii ni mbaya jaribu kuruka ruka zawadi nyingine mpe hata ukiwa hujasafiri, au siku nyingine ukisafiri unarudi mikono mitupu au unambadilishia zawadi ili usimjengee mazingira ya kukariri. Madhara ya yeye kukariri zawadi ni makubwa sana kwasababu yeye anajua mpenzi wangu akisafiri lazima aniletee kitu fulani halafu unarudi mikono mitupu unadhani inakuwaje? Kuna wengine wanabwatuka kabisa 'inamaana dear hujaniletea zawadi yeyote?" mwingine hasemi kitu anajifanya yuko sawa ila utaona ghafla mapokezi na ule uchangamfu wake ghafla unapotea.Nadhani wote mnaelewa mapenzi ya sikuhizi yapoje

Pamoja na hayo yote mpe mpenzio zawadi hata pipi ni zawadi banaaa! Na wewe unayepewa zawadi jifunze kushukuru!

Sijamlenga mtu yeyote hili ni wazo tu lililonijia leo, usije ukaanza kuleta zawadi japo nitapokea heheheeeeee! Kama limekuuma kachome ganzi

Monday, August 6, 2012

Wivu uliopitiliza unakera

Hakuna binadamu asiyekuwa na wivu kwa mtu ampendaye ila ukizidi unaharibu hata hayo mapenzi yenyewe.

Utakuta mtu anamfuatilia mpenzi wake hadi kufikia hatua ya kumtumia watu ili wamtongoze ajue kama huyo mpenzi wake mwaminifu au lah sasa ukikutana na mshenzi mwingine huyo uliyemtuma anatembea naye na wewe anakumwaga vilevile,
Pia kuna wale wa simu, akikupigia akikuta simu busy tu ugomvi sasa yeye hana ndugu, jamaa na marafiki? kwenye hiyo simu kuna namba yako wewe tu? na hawa wanatabia ya kushika sana simu za wapenzi wao ikiingia sms wa kwanza utafikiri simu yake au simu ikiita tu utaona alivyotoa mijicho kama mjusi aliebanwa na mlango.

Japokuwa wanasema mapenzi bila wivu hakuna mapenzi ila mi nakwambia, ukiwa na wivu uliopitiliza unakuwa kero kwa mpenzio so jitahidi uwe na wivu ule wa kibinadamu usitake kuchunguza chunguza sana au kusikiliza ya watu wanayoongea nje, msikilize mpenzio na jifunze kuamini kile cha mdomoni mwake hata kama unahisi anakudanganya we muitikie tu coz atajichanganya tu na ukweli utajulikana.

Halafu nikwambie siri yule anayejifanya anakuonea wivu sana na kukuchunguza  chunguza jua kuna kitu nyuma ya pazia kuna uovu anaufanya sasa anahisi na wewe unafanya hivyohivyo.

Angalizo: si wote wenye wivu uliopitiliza wanamambo wanafanya nyuma ya pazia wengine ndo hivyo wamezaliwa


Ila kwa ushauri wangu hakuna binadamu asiyekuwa na wivu hata mimi mwenyewe nina wivu sana, ila tu punguza wivu kidogo jaribu kumtrust mpenzi wako japo kidogo, wivu ukizidi ni kero. Siku ukiona kama unachezewa rafu kabisa sasa hapo fanya mchakato.

BATA UKIMCHUNGUZA SANA HAUTAMLA!

Thursday, August 2, 2012

Huyu ndiye mwenye tatoo nyingi duniani

Julia Gnuse
Kama wewe unajiona una matatoo mengi basi hujamfikia huyu mwanadada,
Jina lake ni Julia Gnuse, 95% ya mwili wake umechorwa tatoo na tatoo zote amechora kwa artist mmoja.

Tarehe 26 May 2010 Julia alivunja record kwa kuandikwa kwenye kitabu cha 'Guiness World Records'

Wednesday, August 1, 2012

How to get pregnant with twins


Am not sure if it’s true but I have wrote this so that you can read and gain something from it,so don’t ask JT  so many questions.


FOREVER BLESSED CASSAVA SUPPLEMENT FOR TWINS

How can you get pregnant with twins naturally?  Consider using our all-natural Cassava supplement.

"WHAT IS CASSAVA AND HOW CAN IT HELP ME HAVE TWINS?":

The Yoruba tribe in West Africa has the highest rate of twinning in the world. A study concluded that the mother's diet was the cause, being high in Cassava. The peelings and roots of this vegetable contain a chemical that causes hyper-ovulation. This is the same method that is used by prescription drugs to increase the chances of twins and overall fertility.

Our Cassava supplement is a welcome, all natural alternative to drugs.

Cassava is an all-natural supplement. It does not matter if you are taking hormones or prescription drugs at the same time. It also does not matter what time of the month you start to take the supplement. Cassava supplements have had no reported side effects.

The Yoruba tribe described as having the highest percent chance of twins in the world eat the whole Cassava plant every day. It is a staple of their diet.

Our Cassava supplement is concentrated powdered Cassava Root and Peelings. The Cassava itself only contains a very small amount of the substance in comparison with the roots and peelings. Since the Yoruba people eat the entire Cassava plant they get about 900mg of the peelings and root per day.

Our product is made to replicate exactly that, 900mg per pill of concentrated powdered Cassava root & peelings.

The longer the supplement is taken the greater the chance of twins, with the maximum chances of twins being reached after only 5 months. That percent chance is added to whatever natural chances you already have. (The normal rate of twins is about 1 in every 32 births or 3.1% chance.) After taking Natural Cassava supplement your chances can reach 50% or more!


If you can’t eat Cassava direct there are some capsules u can use instead

Product Name : 100% Cassava Supplement | 30 Day Supply

This product is made directly from the Cassava plant. There are no additives, just pure natural powdered Cassava.

Directions: Take 1 capsule daily to induce hyperovulation. This will increase overall fertility and dramatically increase the chances of twins.

To Order product visit www.foreverblessestwins.com