Wednesday, October 24, 2012

Unajua utamu wa denda???Nakujuza sasa

Nitashindwa kukuelewa wewe ambaye mnaanza tu kukukuruka na mpenzio au mkeo/mumeo bila hichi kitu 'denda' au french kiss

Bwana asikwambie mtu denda lina raha yake, denda lina uwezo uwezo wa kuhamisha fikra kutoka upande mmoja hadi mwingine. Mfano mkeo/mumeo kuna kitu kimemuudhi muombe msamaha huku unamsogelea taratibu halafu ukimfikia mpe ulimi uone, yani automatically hasira zooote zinakatika naye utaona atakavyojibu mapigo na mwisho wa siku mnajikuta hata mkimaliza mchezo kabisa.

Siwezi kuficha mimi mwenyewe JT ni mbovu sana wa hiyo kitu yani nikipewa denda tu mwili wote wanilegea sasa siyo kwangu tu asilimia kubwa ya watu wote wapo hivyo hata wewe mwenyewe najua utakuwa upo hivyo.



Sasa denda linakuwa tamu zaidi kama wote midomo yenu ni misafi isiyotoa harufu, sidhani kama utaenjoy endapo mwenzako kinywa kinatema mmmmh hapo ndo utakuta wengi hawapendi kukiss wapenzi wao, sasa kwanini ukose na umkoseshe raha mwenzio kwa kitu kidogo hivyo?? Kuna wengine mna matatizo ya kunuka mdomo basi hakikisha unamuona mtaalam ndugu yangu bila hivyo utaaibika na kujua kama unanuka mdomo ni rahisi sana sogeza kiganja chako mdomoni na utoe hewa wewe mwenyewe utaisikia au nyonya kidole chako halafu nusa, harufu lazima ibaki kwenye kidole kama una huo ugonjwa nenda kwa wataalam ila vinginevyo jitahidi kupiga mswaki mara kwa mara kwa dawa maalum pia kama penda kutafuna BIG G mara kwa mara hii kidogo itasaidia kupoteza harufu. Au siku hizi kuna manukato ya mdomo pia waweza tumia

Pia kingine ambacho napenda niwaambie usije ukatoka kula samaki, dagaa au karanga halafu bila hata kusafisha mdomo ukaenda kumpa denda mpenzio nikwambie ukweli unampa kero sababu harufu ya hivyo vitu hufanya mdomo utie kichefuchefu,so safisha kwanza mdomo au tafuta hata big g halafu ndo mambo yaendelee usimpe shombo mwenzio wengine wanakinyaa eeenh?

CHOMA GANZI!
Haya hilo ndo la leo la kumoyo 'denda linautamu wake jamani' dah! haswa umpate anayelijulia mbona utadata!

Mi ndo nishalopoka likikuuma kama kawaida choma ganzi!!

5 comments:

  1. Jesca wewe ni mtundu sana! anayelijia denda hufanyaje?

    ReplyDelete
  2. Ya kweli hayo leo nitakujaribu nione kama kweli nikikupiga denda utalegea....Mdau wa gezaulole na chadibwa

    ReplyDelete
  3. Sasa utanipigaje denda wakati mimi nina wangu, mbona wataka kunivunjia ndoa mie mzee wa Geza??

    ReplyDelete
  4. Nakubali raha ya denda

    ReplyDelete