Naomba msome kwa umakini na mnisaidie kutoa ushauri kwa huyu dada, ambaye yuko njia panda
Nina bf wangu ambaye tuna mahusiano ya muda mrefu kidogo, mpenzi wangu mimi yuko busy sana kwasababu ya majukumu hivyo kuonana kwetu ni kwa nadra sana, inaweza ikapita miezi 2 nisimtie machoni hapo ni kumuona tu kwenye swala la mapenzi ndo kabisaaa inaweza pita hata miezi 3 ila shida zangu za kifedha zote ananitatulia hata kama ni kodi ya nyumba ikiisha atatuma M-Pesa,
Sasa kinachonitatiza mimi ni kwamba hivi karibuni ametokea mume wa mtu ambaye naamini kuwa ananipenda, anatumia muda wake mwingi kuwasiliana na mimi na kuwa na mimi kwakuwa mpenzi wangu yuko busy sana yeye ndo huwa ananipa company siku zote na mbaya zaidi mapenzi yangu yamezidi kwake kuliko haya kwa bf wangu, mara zote anakuja yeye kwanza mbele ya bf wangu kwenye kichwa changu.
Ananipa kila ninachokitaka anaridhisha kwa kila jambo na ananielewa sana, hata kama sijamwambia kitu yeye huwa anakuwa tayari ameshafikiria na kujikuta napata kile ninachokihitaji, kiukweli uwezo wake kitandani ni mkubwa unaoniridhisha sana ananipa mahaba yote na ananifikisha ipasavyo.
Naomba nieleweke kuwa sijampendea pesa huyu kaka bali mapenzi anayonipa najisikia raha sana kila nikiwa naye imefikia hatua hata siogopi tena kufumaniwa na bf wangu, na kama akipiga simu niko naye naweza hata nisipokee naona kama ananipunguzia radha. Kusema ukweli sina maneno ya kudhihirisha ninachokipata kutoka kwa huyu mume wa mtu ila kiukweli nampenda sana, na naiheshimu sana familia yake na naomba Mungu mkewe asigundue sababu itakuwa imeniharibia.
Jamani naombeni ushauri wenu nifanyeje?? Kwani kwasasa nataka niachane na bf wangu ili niwe na mume wa mtu peke yake. Nishaurini jamani niko njia panda!
Kama una ushauri weka hapo chini, au nitumie kwa tarimojesca@gmail.com au kwenye page yangu ya facebook au twitter.

Jesca kumbe unanicheat mimi!! sikujua kama wataka kuniacha!!!
ReplyDeleteHahahahaaaaaa ebu acha kufurahisha wadau
DeleteJamani sikujua kama nakulidhishaga hivo kitandani!!
ReplyDeleteJamani sio mimi ni mtu mwingine!!! msifurahishe macho ya watu
Deletemmmmh pole 1 day utakuja juta kwa unayoyafanya leo ushasema mume wa ..... na sio mume wangu kamwe kaa ukijua hana malengo na ww
ReplyDeleteduh hii inaniusu sana ntafumaniwa nini ivi karibuni......
ReplyDeleteMme wa mtu sumu ishi nae kwa malengo
ReplyDeleteTupo wengi Jesca bt ukwel n kwamba mume wa m2 si wako hata iweje bora ukae nae mbal lasvyo utakuja kujuta......he cant leave his family fir you.....Chukua Hatua
ReplyDelete🌹 Ushuhuda Wangu Kuhusu Dkt. Dawn – Mtu Aliyerejesha Nyumba Yangu na Furaha Yangu
ReplyDeleteNataka kushiriki ushuhuda wangu wa dhati kuhusu jinsi Dkt. Dawn alivyobadilisha maisha yangu kabisa.
Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na alikuwa ameenda kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.
Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwangu — na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.
Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.
Lakini si hayo tu — Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyokuwa ikizunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.
Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote — huzuni, bahati mbaya, au mkanganyiko — usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.
Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com